FISI WAZUA GUMZO NA KUWA TISHIO KAHAMA

Kundi kubwa la  wanyama aina ya fisi limewajeruhi watu  watano  sehemu mbalimbali za miili yao katika  kata za  Nyandekwa na Kilago halmashauri ya mji wa Kahama mkoani Shinyanga wakati wakijaribu kupambana na fisi hao waliovamia makazi ya watu.

Diwani wa Kata ya Kilago PETER EMANUEL amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia  April 28,2019  ambapo  majeruhi watatu hali zao bado hazijaimarika na wanaendelea na matibabu katika hospitali ya mji wa Kahama  na kwamba wananchi katika maeneo hayo amejawa na hali ya wasiwasi.

Wakizungumza wakiwa wamelazwa katika hospitali ya mji wa Kahama, baadhi ya  majeruhi wameiomba serikali  kuwadhibiti fisi hao kwani wanaweza kuleta madhara makubwa kwa wananchi na kwamba wamekuwa wakipambana nao mara kwa mara.

Afisa maliasiri  halmashauri ya mji wa Kahama, THOMAS MANUMBU amesema  tatizo la Fisi kuvamia makazi ya watu   bado lipo kwa wingi katika kata za pembezoni tangu mwezi wa pili mwaka huu  huku akiwataka wananchi kuchukua tahadhari wakati serikali inaendelea kupambana na  fisi hao.

Kwa upande wake Mhifadhi wa wanyanama Tanzania  (TAWA) wilaya ya Kahama, MAPANYA KARUTO  amewataka wananchi kutumia toshi nyakati za usiku na kwamba waondokane na imani za kishirikina  dhidi ya uwepo wa fisi hao.

 Credit - Kahama Fm



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527