MCHUNGAJI ALIYEFUFUA MTU ATAKIWA KUMFUFUA MANDELA



Baada ya sakata lake la kumfufua mtu kutinga kwenye vyombo vya habari na kuzua gumzo katika bara zima la Afrika, Mchungaji Alph Lukau sasa ametakiwa na mchungaji mwenzake kumfufua Rais wa kwanza wa nchi hiyo, Nelson Mandela.

Mchungaji huyo wa kanisa la Alleluia Ministry la Afrika Kusini, ametakiwa kufanya hivyo na mchungaji mwenzake anayejulikana kwa jina la Paseka Mboro Motsoeneng maarufu kama Pastor Mboro, baada ya kwenda kanisani kwake kumtaka atoke nje na kulitolea majibu suala hilo lililoleta mtafaruku kwenye imani.

“Kwa nini unakimbia kama siko sahihi!?, nataka ujisalimishe na uombe radhi. Naweza kuuona uongozi wa kanisa!?. Labda naweza kuombewa na mimi, nataka kumuita mchungaji na tuende kwenye kaburi la Mandela ukamfufue”, amesema Pastor Mboro kwa hisia huku waumini wa kanisa hilo wakitawanyika.

Licha ya maneno hayo huku watu wakiwa wamejaa nje ya kanisa lake, mchungaji Lukau hakutaka kujitokeza, na kuzidi kupandisha hasira za waliofika kanisani hapo, huku wakimtuhumu kuidhalilisha imani ya dini ya Kikristo, na kwamba anadanganya umma kwa kutumia jina la Mungu.
Mchungaji Mboro akiwa nje ya kanisa la Mchungaji Alph Lukau akimuomba atoke nje na kuomba radhi kwa kudhalilisha dini.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527