MKUBWA FELLA AWAJIA JUU WANAOMTUKANA MAREHEMU RUGE

Mtendaji Mkuu wa Mkubwa na Wanawe Youth Organization Mkubwa Fella ameamua kufunguka kuhusiana na ukaribu aliokuwa nao na Marehemu Ruge Mutahaba pamoja na taarifa za msiba kumuumiza kutokana na wawili kujuana tokea mwaka 1995 na kusaidiana vitu vingi.

Fella ameongeza na kusema kuwa watu kwenye mitandao inabidi waache kutukana kwa sababu Marehemu Ruge ana mchango mkubwa kwenye maisha ya muziki na walikutana hata kabla ya Ruge kwenda kwenye matibabu na hivyo cha muhimu ni kumuombea.

“Najua tumeumia wengi na kila mtu anajua uchungu wa kuondokewa mfano mie najua uchungu wa kufiwa na baba, mama mpaka mtoto machungu yote nimepitia kweli msiba unauma alafu kati ya watu wa karibu na Ruge kati ya watu wake 10 sikosi kwani alijua umuhimu wangu nami nilijua umuhimu wake sasa kwa msiba wa mwanangu bosi wangu nimeumia ila nami nipo kwenye ibada napitia naumwa ila naona wapenda ukolofi wanatukana sijuhi wao wanaitaji nifanyeje chengine


“Namini mie na marehemu tunajuana kuliko wewe unaepita kwenye ukurasa kutukana watu unajua vita ngapi tulipigana kuusogeza mziki huu na tasnia hii nimejuana na Ruge 1995 mpaka leo sasa usilete utashi wa biashara kutukana watu mie nilipata bahati kuagwa na brother na wakati anatarajia kwenda kwenye matibabu kabla ajazidiwa yeye ndio alinambia kijana wako mmoja kwenye ya moto atakusumbua ila kuwa makini tena akanisifu najua moyo wako mpana utashinda


“Kuna siku alinambia Fella nikirudi salama napenda tukae tujue tunajengaje mnara timilifu sasa wewe mwenye account yako ya kutukana watu sio vizuri msiba ni mkubwa alafu kulia kila mtu anakilio chake sasa usikae ukaona unavyo lia wewe na mwengine uwe sawa lakini najua yatapita ila nakumbuka baba yangu alifariki 2006 siku iyo ilikuwa Fiesta Arusha nimetoka home alfajiri natua Arusha napigiwa mzee kafariki nakumbuka Boss Kusaga na Ruge walinambia usiuzunike siku hii ila sema asante


“Mwenyezi Mungu kwa kunipatia ili kuiona siku ya mwisho ya baba sasa kama nilipewa mawaidha aya na nikashinda sasa ili la msiba wa boss Ruge muhimu naona ni kumuombea kwa mwenyezi Mungu amuweke pahala pastahiki. nasi tunae subiri time yetu tuwaombee dua marehemu wetu wote tuseme Inshaallah pia instar iwe kipasha habari isiwe ibada eti umu kama ndio mwenyezi Mungu anakagua. kweli wakati mgumu ila tuikaribishe subraaaaa na Inshaallah mwenyezi Mungu tuongoze Amen"
Advertisement

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527