LIPUMBA ATOA ONYO KWA WANAOPORA MALI ZA CUF NA KUHAMA NAZO ACT- WAZALENDO


Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amesema chama hicho hakitawavumilia wanaopora mali za chama hicho na kuzihamishia Chama cha ACT Wazalendo.

Akizungumza na wandishi wa habari leo Jumanne Machi 19, Jijini Dar es Salaam, Profesa Lipumba amesema hatua hiyo ni utapeli na wizi wa wazi, hivyo chama chake kitafuata utaratibu wa kisheria kuzirejesha.

“Hili ni jambo la kisheria, mali za chama zitaendelea kuwa za chama, hao wanaobadili rangi majengo ya chama ninawaambia, akili za Maalim Seif wachanganye na zao, kwa sababu jinai itawahusu wao binafsi na huyu maalim hatakuwa nao,” amesema Profesa Lipumba.

Aidha, Profesa Lipumba amesema kuna watu wenye fikra nzuri ambao walikuwa wanaungana na Maalim Seif lakini hawawezi kubadilisha maamuzi yao na kumfuata ACT.

“Nataka kuwambia wale wote ambao mlikuwa sambamba na Maalim Seif wenyeviti, madiwani, wabunge na wanachama wa CUF tujumuike na tuwe pamoja katika kukijenga chama chetu,” amesema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527