NCHI NZIMA YAKOSA UMEME KWA SIKU TANO


Picha ya giza mjini Caracas.
Shughuli mbalimbali ikiwemo shule na ofisi za serikali nchini Venezuela, zimesitishwa kwa saa 48 kuanzia jana Machi 11, 2019, kutokana na kukosekana kwa umeme nchi nzima tangu alhamisi mchana Machi 7, 2019.

Rais wa nchi hiyo ya Amerika ya Kusini, Nicolas Maduro ameishutumu Marekani kuwa ndio walioshambulia miundombinu ya umeme, japo amekiri kuwa hawajathibitisha hilo bado.

Kwa mujibu wa kiongozi wa upinzani nchini humo Juan Guaido, mpaka sasa ikiwa inakaribia siku ya 5, baadhi ya maeneo muhimu hayana umeme ikiwemo hospitali na watu takribani 17 wamepoteza maisha kwa kushindwa kufanyiwa upasuaji.

Imeelezwa kuwa hitilafu kubwa imetokea katika mitambo mikuu ya kuzalisha umeme katika mji mkuu wa Venezuela Caracas hivyo kusababisha kukosekana kwa umeme katika eneo kubwa la nchi.

Maduro ameendelea kusisitiza kuwa umeme utarejea taratibu katika maeneo ya Caracas na kwingine huku akiweka wazi kuwa huo ni mpango wa upinzani kumwondoa madarakani kwa kushirikiana na nchi za Marekani na Ulaya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527