WILAYA YA MUFINDI YAANZA KUPIGA KURA KUWABAINI WABAKAJI NA WALAWITI

Na.Amiri kilagalila
Halmashauri ya wilaya ya Mufindi mkoani Iringa imeanza kupiga kura ya maoni ya siri katika vijiji vyote vya tarafa tano za wilaya hiyo ili kuwabaini waharifu wa matukio ya ubakaji na ulawiti ambayo yanaonekana kukithiri katika wilaya hiyo na kuifanya wilaya hiyo kuwa ya kwanza kati ya wilaya tatu za mkoa huo kwa ukatili huo.


Kaimu katibu tawala wa wilaya ya mufindi Joseph Mchina amesema kuwa kura ya siri ya maoni imeanza tangu januri katika vijiji na mitaa na baadae litafanyika katika taasisi za elimu zikiwemo shule za sekondari , msingi na vyuo ili kuwabaini watu wanaohusika na matukio hayo.


Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa mafinga mh Charles makoga amesema kuwa sababu za matukio ya kikatili ya ubakaji na ulawiti katika mkoa wa iringa zinachagizwa na imani za kishirikina mambo ambayo yanatokana na ukosefu wa elimu.


Badhi ya wananchi waliozungumza na mtandao huu wamesema utaratibu wa serikali kupiga kura ya maoni ya siri uende sambamba na uandaaji wa takwimu sahihi kwa kuwa bado kunataarifa zilizipo hazina uhalisia na matukio.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527