NDOO 226 ZENYE SAMPULI ZA MIAMBA YA MADINI 883 ZAKAMATWA MWANZA


Kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Mwanza inalishikilia gari lori aina Fuso lililokuwa likisafirisha shehena ya sampuli za madini kutoka mkoani Geita kwenda jijini humo.

Mwenyekiti wa kamati hiyo mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella jana alisema gari hilo lilikamatwa jana na ndoo 226 zenye sampuli za miamba ya madini 883 mali ya Mgodi wa Dhahabu Geita (GGM).

“Gari hilo lilikamatwa na askari waliokuwa doria baada ya kubaini wahusika walikuwa na upungufu wa vibali vinavyoruhusu kusafirisha mzigo huo kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine,” alisema.

Mongella alisema shehena hiyo ilikuwa ikisafirishwa kwenda kwenye maabara ya kupima madini hayo ya SGS iliyopo jijini Mwanza.

Kutokana na hali hiyo, mkuu huyo wa mkoa aliagiza kuchunguzwa na kufuatilia uhalali wa sampuli hizo huku akiwataka watendaji wa Serikali kufanya kazi kwa uadilifu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527