MWIZI APEWA ADHABU YA KULA PILIPILI

 Baadhi ya wakazi Mombasa nchini Kenya sasa wameanza kuitumia pilipili kama kifaa cha kuadhibia watu wanaokutwa na makosa kwa mfano wizi.

Katika video ambayo sasa inasambaa kwa kasi mtandaoni na kufuatiliwa na watu mbalimbali, jamaa anayedaiwa kuiba jozi ya viatu alilazimishwa kula pilipili.

Haijafahamika ni viatu vya aina gani alivyoiba kabla ya kupewa adhabu hiyo.

 Waliomkamata katika tendo hilo walimlazimisha kukiri kuiba kabla ya kumpa pilipili hiyo kuila na kumtaka aseme hatowahi kurudia tena. 

 "Mimi ni mwizi na mimi huiba viatu, nilitumwa na Felix anayefanya kazi feri. Baadhi ya viatu ninavyoiba sisi huviuza feri na Changamwe," alisema mwizi huyo chini ya ulinzi mkali.

 Hata hivyo hii sio mara ya kwanza kwa adhabu ya aiana hii kutumika na itakumbukwa katika kisa kingine cha wizi, jamaa alitakiwa kuchagua kati ya kupigwa kitutu na kula pilipili.

 La kushangaza ni kuwa, jamaa huyo alichagua kula bakuli la pilipili huku waliokuwa wamemkamata wakiangalia. 

BOFYA HAPA KUONA VIDEO YA JAMAA AKILA PILIPILI
This shoe thief will never steal again after being forced to eat pilipili 😂😂😂


1:38
15.8K views

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527