BINTI ALIYETAKA KUWA MKE WA PILI AUAWA KWA KUCHOMWA SEHEMU ZA SIRI

Binti aliyejulikana kwa jina la Joyce Jackson (18) mkazi wa kijiji cha Rusega kata Karenge wilayani Biharamulo, mkoani Kagera ameuawa kwa kuchomwa na vitu vyenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo sehemu za siri. 

Inaelezwa kwa tukio hilo limetokea Februari 8,2019 majira ya saa moja asubuhi ambapo agundulika kuwa ameuawa ndani ya nyumba alimokuwa akiishi. 

Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Revocatus Malimi Joyce alivamiwa na watu wasiojulikana na kumchoma na vitu vyenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo sehemu za siri.

 Inadaiwa kuwa binti huyo alikuwa katika mipango ya kuolewa na Balushamina Mtondo kama mke wa pili. 

Tayari jeshi la polisi wanamshikilia mke wa kwanza wa baba huyo Jenesia Jacobo (29 ) kwa mahojiano zaidi kuhusiana na mauaji hayo.

Na Mwandishi wa Malunde1 blog 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527