MTOTO ALIYEKATWA KOROMEO NJOMBE AFARIKI DUNIA


 . Meshack Myonga (4), aliyenusurika kuuawa baada ya kutekwa na kukatwa koromeo wilayani Njombe amefariki dunia leo mchana Jumamosi Februari 9, 2019 katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.

Desemba 23, 2018 mtoto huyo alitekwa na mtu asiyejulikana akiwa nyumbani kwa wazazi wake mtaa wa Mji Mwema wilayani Njombe, kisha kupelekwa msituni na kukatwa koromeo kabla ya kuokolewa na kijana mmoja.

Baada ya kuokolewa alipelekwa Hospitali ya Mkoa ya Kibena-Njombe na baadaye kuhamishiwa hospitali ya rufaa Mbeya kwa matibabu zaidi.
Na Godfrey Kahango, Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post