MSIMU WA SITA WA COKE STUDIO WAZINDULIWA


Mkurungezi mkuu wa Coca cola Kwanza Basil Gadzios akizungumza na wageni waliofika kuhudhuria uzinduzi wa msimu wa Sita wa Coke Studio iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Mkurugenzi wa mauzo na masoko, wa CocaCola Kwanza, Josephine Msalilwa akizungumza na wageni waliofika kuhudhuria uzinduzi wa msimu wa Sita wa Coke Studio iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Msanii Nandy akiimba huku akicheza na Mkurungezi mkuu wa Coca cola Kwanza Basil Gadzios wakati wa azinduzi huo.
Msanii Harmonize akizungumza katika uzinduzi huo. Wengine ni Rayvan, Jux na Nandy.
Wageni waalikwa wakifuatilia.
Msanii Jux akitoa burudani.
Wageni waalikwa wakifurahia.
Msanii Harmonize akifanyiwa mahojiano na wanahabari.
Mtangazaji wa Times Redio, Lil Ommy akipata selfie na msanii Jux.
Dj D-Ommy akitoa burudani huku shabiki akijiachia.

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.

Msimu Mpya wa Coke Studio Africa umezinduliwa rasmi Tanzania katika halfa iliyofanyika klabu ya burudani Lifepark Mwenge.

Tanzania itawasikilishwa na wasanii watano watakaotumbuiza katika msimu wa sita wa Coke Studio.

Akizungumza mbele ya wageni waalikwa Mkurungezi mkuu wa Coca cola Kwanza Basil Gadzios amekiri kufurahishwa vipaji na uwezo wa wasanii watanzania watakao shiriki kwenye msimu huu mpya.

Kwa upande wake mkurugenzi wa mauzo na masoko wa Cocacola Kwanza, Josephine Msalilwa, akizungumza wakati wa kuwatambulisha wasanii hao kuwa ni Faustina Charles' Nandy', Raymond Mwakyusa'Rayvanny', Rajabu Abdul'Harmonize', Juma Jux na Mimi Mars.

Amesema wasanii hao wataungana na wasanii wengine 20 kutoka nchi mbalimbali za Afrika na kutimiza idadi ya wasanii 25 watakaokuwa katika msimu wa mwaka huu.

"Nchi nyingine msanii huchukuliwa mmoja lakini kwa Tanzania imekuwa tofauti kidogo, hii yote inaonesha ni namna gani muziki Watanzania yani bongo fleva umekuwa ukikubalika na wasanii wake kupendwa," amesema Josephine.

Nao wasanii akiwemo Rayvanny amesema anashukuru kuwa mmoja wasanii watakaotumbuiza katika msimu huu huku akieleza hii ni mara yake ya pili.

Msanii Nandy amesema kushiriki Coke Studio 2019 kunakusaidia kukutana na wasanii kutoka Africa wenye vipaji lukuki... nafasi hii kwa msanii yoyote ni kitu cha kujivunia sana na pia inasaidia kutengeneza kazi tofauti na kufanya jina au brand ya msanii kuimarika na nguvu katika soko la muziki Afrika na dunia nzima.

"Coke Studio ni kitu kikubwa, na hakuwahi kutegemea kukutana na msanii mkubwa kama Skales kutoka nchini Nigeria ambaye ameurudia wimbo wake wa Ninogeshe na kunuelezea kuwa ni msanii ambaye ana ushirikiano mzuri," amesema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post