MAMA MBARONI KWA KUMCHOMA MTOTO ALIYEDOKOA CHAKULA

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linamshikilia Eliza Denis (23) mkazi wa Makulu mkoani hapa kwa tuhuma za kumpiga sehemu mbalimbali za mwili na kumchoma moto mikononi mtoto wake wa kambo, Jackson Denis (5) kwa madai ya kudokoa chakula.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba Jeshi la Polisi linamshikilia mama huyo.

Kamanda Muroto alisema watu wamekuwa wakiendelea kujihusisha na matukio ya ukatili wa kijinsia, hususani kwa watoto hivyo Jeshi la Polisi halitasita kuwachukulia hatua kali za kisheria.

“Huko maeneo ya Dodoma Makulu amekamatwa mama mmoja ajulikanae kwa jina la Eliza Denis ambaye ni mkulima na mkazi wa Dodoma Makuli kwa makosa ya kumpiga sehemu mbalimbali za mwili na kumchoma mikononi mtoto wake wa kambo aitwae Jackson Denis mkazi wa Dodoma Makulu,” alisema Kamanda Muroto.

Alisema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani kujibu shtaka hilo siku za hivi karibuni.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527