BUNGE LAREJEA BAADA YA VING'ORA KUZUA TAHARUKI

Saa moja baada ya kikao cha Bunge kuharishwa kutokana na taharuki iliyotokana na ving’ora kulia, Spika wa Bunge Job Ndugai amesema mpaka sasa hawafahamu chanzo cha tukio hilo.

Kabla ya kuahirishwa kwa kikao cha Bunge saa 5:03 asubuhi kilikuwa kikiongozwa na mwenyekiti wa Bunge, Najma Giga.

“Nawapeni pole. Hadi sasa hivi hatujajua chanzo tutakapojua tena baadaye tutaelezana sababu ya kulia kwa ving’ora,” amesema.

Amesema kama kuna maswali (ya wabunge) yamebaki watayafanyia utaratibu huku akiwapa pole wabunge na kwamba wataalamu wanaendelea kufanya uchunguzi.

Licha ya wabunge kuambiwa waingie ndani ya ukumbi saa 5:31 asubuhi lakini kikao kilichelewa na kuanza saa 6:03 mchana.

“Kulikuwa kumebakia maswali mawili hayajajibiwa,” amesema Ndugai na kuongeza: “Tutayafanyia utaratibu siku zijazo.”

Wenyeviti wa kamati wanaosoma taarifa zao wameambiwa wasome kwa dakika 30 kila mmoja badala ya dakika 45.
Na Sharon Sauwa, Mwananchi 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527