WAZIRI JAFO ATOA SIKU 68 KWA HALMASHAURI KUREJESHA FEDHA


Waziri wa nchi,Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo ametoa siku 68 kwa halmashauri 4 za Kigoma Ujiji, Butiama, Liwale na Bahi kurejesha fedha za mradi wa elimu (Equip)zilizotumika kinyume na utaratibu.


Aidha ameelekeza mamlaka ya nidhamu kumchukulia hatua za kumuondoa kwenye nafasi yake afisa mipango wa halmashauri ya Bahi kutokana na kushindwa kutimiza wajibu wake.

Halmashauri hizo ni kati ya halmashauri 8 zilizotumia fedha kinyume kiasi cha milioni 912.7 ambapo halmashauri 4 zilitekeleza agizo lake na kurejesha fedha.

"Halmashauri hizi wamenihuzunisha sana kwa kutotii maelekezo, naziagiza mpaka machi 28 mwaka huu wawe wamerejesha ili fedha hizo zitekeleze miradi iliyokusudiwa, "amesema Jafo

Mbali na hayo amemuagiza Naibu Waziri wake Mwita Waitara kuwa mkali katika kusimamia miradi ya elimu agizo ambalo Waitara ameahidi kulishughulikia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527