RAIS TRUMP AONDOKA KWA HASIRA KWENYE MKUTANO NA WANADEMOCRATICS

Rais Trump wa Marekani anaelekea katika mpaka na Mexico ikiwa ni sehemu ya juhudi zake za kujenga ukuta,siku moja baada ya kutoka katika mkutano wa majadiliano wakati wapinzani wa ujenzi huo kutoka chama cha Democratic 

Donald Trump alivurumuka na kutoka katika mkutano na viongozi wa mabaraza ya bunge la Marekani " nilisema kwaheri," aliandika katika ukurasa wa Twitter muda mfupi baada ya mkutano huo, wakati juhudi za kumaliza kufungwa kwa sehemu shughuli za serikali, ziliingia katika mparaganyiko mkubwa. 

Mamia kwa maelfu ya wafanmyakazi wa serikali wanakabiliwa sasa na kukosa mishahara hadi kesho Ijumaa.


Wakati atakaposimama kwa muda leo mjini McAllen , Texas , Trump atafanya ziara katika kituo cha mpakani cha doria kwa ajili ya mazungumzo kuhusiana na uhamiaji na usalama wa mpakani, na kupata maelezo kuhusu usalama wa mpaka.

 Lakini Trump ameelezea shaka shaka yake kwamba kujitokeza kwake pamoja na matamshi hayatabadilisha mawazo ya mtu yeyote, wakati akitafuta kupata dola bilioni 5.7 kwa ajili ya ujenzi wa ukuta ambao umekuwa ni ahadi yake kuu tangu alipokuwa akifanya kampeni ya urais.

Mazungumzo hayo yalizusha uvumi zaidi juu ya iwapo Trump atatangaza dharura ya kitaifa na kujaribu kuidhinisha ujenzi wa ukuta huo binafsi iwapo baraza la Congress halitaidhinisha fedha anazotaka.

Chanzo:DW

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527