TRUMP AIONYA UTURUKI DHIDI YA WAKURDI

Vikosi vinavyoungwa mkono na Uturuki wako tayari kushambulia wapiganaji wa Kikurdi kaskazini mwa Syria.

Rais wa Marekani Donald Trump ametishia 'kuiangamiza Uturuki kiuchumi' iwapo taifa hilo litavishambulia vikosi vya wakurdi nchini Syria baada ya wanajeshi wa Marekani kuondoka Syria.

Katika ujumbe wake alioutuma kwenye mtandao wa kijamii Twitter, Trump amesema hakutaka Wakurdi kwa upande wao nao pia waichokoza Uturuki.

Vikosi vya Marekani vimepambana kwa ushirikiano na wanamgambo wa Kikurdi kaskazini mwa Syria dhidi ya kundi la Islamic State (IS).

Uturuki hatahivyo inatazama wapiganaji hao wa vitengo vya YPG kama magaidi.

Rais Recep Tayyip Erdogan amezungumza kwa hasira kuhusu Marekani kuliunga mkono kundi hilo, na kuapa kuliangamiza.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527