TATIZO SUGU LA SIMBA NA YANGA LAITAFUNA AFRIKA


Klabu ya soka ya Simba inawakilisha nchi kwenye michuano ya kimataifa na tayari ipo katika hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa Afrika ikiwa inaongoza kundi D, baada ya kushinda 3-0 dhidi ya JS Saoura.


Pamoja na kuwakilisha nchi lakini, Simba inaacha manyanyaso kwa vilabu vingine vinavyoshiriki ligi kuu ya soka Tanzania bara ambavyo havijui lini vitacheza mechi zake dhidi ya klabu hiyo ambayo tangu ianze kucheza mechi za kimataifa imejikusanyia viporo takribani 6.

Wiki hii ambapo baadhi ya timu zitakuwa zinacheza mzunguko wa 21, Simba wao hawatakuwa sehemu ya ratiba hiyo ya ligi kuu kwani watakuwa wanajiandaa kwaajili ya mchezo wa pili wa hatua ya makundi dhidi ya AS Vita Club, utakaopigwa Januari 19 huko DR Congo.

Vinara wa ligi kuu msimu huu, klabu ya Yanga huenda wakawa hawafurahishwi na Simba kuwa na viporo vingi lakini msimu uliopita Yanga walifika hatua ya makundi ya Kombe la shirikisho Afrika na walikuwa na viporo kama ilivyo kwa Simba msimu huu.

AFRIKA
Kwa upande wa timu ziliopo kundi moja na Simba, Al Ahly nao wamecheza mechi 14 tu kati ya 17 ambazo timu nyingine zimecheza huku pia ikiwa haipo kwenye ratiba ya ligi wiki hii ambapo itasafiri kuifuata JS Soura ambayo imecheza mechi 16 kati ya 17 za ligi.

Kwa upande wa DR Congo, AS Vita Club wao wamecheza mechi 14 kati ya 15 za ligi. Nchini Afrika Kusini Mamelodi Sondowns ambao wapo kundi A klabu bingwa Afrika wamecheza mechi 13 pekee kati ya 17 ambazo tayari timu nyingine zimecheza.

Chanzo:Eatv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527