FAHAMU KIKOSI BORA ZAIDI BARANI ULAYA 2018

England walifika nusu fainali katika Kombe la Dunia nchini Urusi mwaka 2018, lakini hakuna mchezaji hata mmoja wa timu hiyo ya taifa aliyejumuishwa kwenye kikosi bora cha wachezaji 11 Ulaya, chaguo la mashabiki kwa mwaka huo.


Ingawa kuna wachezaji watatu wanaocheza Ligi ya Premia kwenye kikosi hicho, hata nahodha wa England Harry Kane aliyeshinda tuzo ya mfungaji bora zaidi Urusi, hajajumuishwa.

Kiungo wa Liverpool Virgil van Dijk na wachezaji wawili wa Chelsea N'Golo Kante na Eden Hazard wamo kwenye kikosi hicho cha wachezaji XI.

Cristiano Ronaldo ni miongoni mwao, ambapo amejumuishwa kwa mara ya 13 sasa, na kuwa mchezaji aliyejumuishwa mara nyingi zaidi.

Mshambuliaji huyo wa Ureno ambaye sasa huchezea Juventus ya Italia, aliisaidia klabu yake ya zamani Real Madrid kushinda Kombe la Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya tatu mtawalia mjini Kiev, Ukraine mwezi Mei ambapo waliwalaza Liverpool.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527