MKUU WA MKOA WA TABORA AWAONYA WANAOUNGANISHA SAUTI NA RAIS MAGUFULI..SOMA HIYOOO

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Aggrey Mwanri amewataka Watu wanaounganisha sauti yake na kuchanganya sauti ya Rais Magufuli, kuacha mara moja tabia hiyo kwani inaleta picha mbaya kwa viongozi.

Mwanri amesema kuwa kitendo hicho sio kizuri, kwani viongozi wa juu kama Rais ni taasisi na mamlaka yake ni kubwa.


Mwanri ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku chache tangu kusambaa kwa kipande kifupi cha video ambayo inamuonesha kiongozi huyo, na Rais Magufuli wakijibishana kwa maneno.


Mwanri amesema; "wakati mwingine huwa naona wanavyotuweka pamoja na viongozi ambao nawaheshimu sana, si kitu kinachonifurahisha sana, licha ya kuunganisha kuleta kichekesho lakini mimi binafsi sifurahishwi nao."


"Kuhusu wanaotumia sauti yangu kutengeneza muziki sina shida nao ila muhimu mimi matokeo yangu ipatikane kwa wananchi wa Tabora na wala sitakimbilia kwenye biashara eti wanilipe." ameongeza Mwanri.


Mkuu huyo wa Mkoa wa Tabora Agrey Mwanri amekuwa maarufu kupitia mitandao ya kijamii hivi karibuni kwa kuanzisha misemo mbalimbali ikiwemo, sukuma ndani, fyekelea mbali, pamoja na Injinia soma hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527