SIMBA MSHINDI WA TATU SPORTPESA..WAMEICHAPA MBAO UWANJA WA TAIFA

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara Simba, leo wameibuka washindi wa tatu katika mchezo wa SportPesa Cup Uwanja wa Taifa kwa kushinda mbele ya Mbao kwa penalti 5-3.

Dakika 90 za mchezo huu ambao ulikuwa na kasi kwa timu zote mashabiki walishuhudia timu zikitoka suluhu na kupelekea mwamuzi kuamua ipigwe mikwaju ya penalti.

Simba walifunga penalti zote tano huku wapigaji wakiwa ni Emanuel Okwi, Pascal Wawa, Deogratius Munish, Nicholas Gyan na Clatous Chama.

Kwa upande wa Mbao waliofunga walikuwa ni Said Khamis, Vincent Philipo na Peter Mwangosi huku Rajesh Kotecha akikosa penalti ya nne.

Kwa matokeo hayo Simba wanakuwa washindi wa tatu wa mashindano ya SportPesa Cup huku Mbao wakishika nafasi ya nne.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527