YANGA NA SIMBA KUPOZA MACHUNGU YA VIPIGO PAMOJA LEO


Wachezaji wa Simba kushoto na Yanga kulia.

Klabu za soka za Yanga na Simba zote zimerejea Dar es salaam usiku wa kuamkia leo, Januari 21, 2019, zikitokea kwenye mechi zake za uganini ambapo zote ziliambulia kichapo.

Timu hizo mbili zote zimeunganisha kwenye maandalizi ya michuano ya SportsPesa ambapo kila timu imeingia kambini kuanza mazoezi tayari kwa michuano hiyo inayoanza kesho.

''Kikosi kimerejea salama jijini Dar es salaam jana usiku na kuingia kambini moja kwa moja tayari kwa maandalizi ya michuano hiyo ambapo mchezo wa kwanza kwetu utakuwa kesho Jumanne dhidi ya Kariobangi Sharks'', imeeleza taarifa ya Yanga.

Kwa upande wake msemaji wa Simba Haji Manara amesema baada ya timu kurejea salama nyumbani, leo inaanza mazoezi kwa ajili ya michuano hiyo, ambapo inatarajia kucheza na AFC Leopards ya Kenya katika mchezo wake wa kwanza kesho Jumanne.

Simba ilikuwa nchini DR Congo ambapo ilifungwa mabao 5-0 na AS Vita Club kwenye mechi ya kundi D Ligi ya Mabingwa Afrika huku Yanga ikifungwa bao 1-0 na Stand United kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post