SIKU ZA CAG ZAHESABIKA

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad.

Ni siku tisa zimebakia kabla ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad, kuhojiwa na Kamati ya Maadili, Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge kama ambavyo alitakiwa kufanya hivyo na Spika Job Ndugai.

Sababu pekee ambayo inamfanya Mtaalamu huyo wa Uhasibu na Ukaguzi kujieleza kwa kamati hiyo, ni juu ya kauli yake kuwa Bunge halifanyi kazi yake kama linavyotakiwa na hasa kwenye kupambana na ufisaidi.

Akitangaza uamuzi wa kumuita kiongozi huyo Spika Job Ndugai alimtaka kufika Januari 21 Dodoma kwa ajili ya kuhojiwa na alisema endapo kiongozi huyo hatofika atatafutwa kwa njia yeyote ili afike kwenye kamati hiyo.

Akijibu swali ambalo lilimfanya ajikute kwenye kadhia hiyo ya kuitwa na Bunge Profesa Assad alisema, 

“kama tunatoa ripoti na kuna ubadhirifu na hatua hazichukuliwi, huo kwangu ni udhaifu wa Bunge. Bunge linatakiwa lisimamie na kuhakikisha kwamba pale penye matatizo, linahakikisha kuwa hatua zinachukuliwa. Sasa, sisi kazi yetu ni kutoa ripoti tu,”

“Na huo udhaifu, nafikiri ni jambo la kusikitisha, lakini ni jambo ambalo tunaamini muda si mrefu litarekebishika. Lakini tatizo kubwa tunahisi kwamba Bunge linashindwa kufanya kazi yake kama inavyotakiwa. Na sitaki kuwa labda nasema jambo hili kwa sababu linahusisha watu fulani, hapana. Lakini nafikiri Bunge likifanya kazi yake vizuri, hata udhaifu ambao unaonekana, utakwisha.” alisema Assad

Chanzo:Eatv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527