NDEGE NYINGINE MPYA YA SERIKALI AINA YA AIRBUS A220-300 KUTUA TANZANIA KESHO

Ndege nyingine mpya ya Serikali aina ya Airbus A220-300 iliyopewa jina la Ngorongoro inatarajia kuwasilini nchini kesho Ijumaa mchana, ambapo itafanya idadi ya ndege zilizonunuliwa na Serikali kufikia sita.

Ndege hiyo ambayo tayari inanakshi za Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) itafanya jumla ya ndege za ATCL kufikia 7, ikijumlishwa na ndege yao ya zamani aina ya Bombardier Q300 ambayo sasa ipo katika matengenezo.

Ndege inayotarajiwa kutua kesho ni ya pili ya aina hiyo, kwani Desemba 23 iliwasili ya kwanza ambayo ilipewa jina la Dodoma. 

Ndege nyingine zinazomilikiwa na shirika hilo ni Bomberdier Q400-8 tatu na Boeing 87-8 (Dreamliner) moja.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527