MANARA KUJICHANGANYA NA MASHABIKI TAIFA LEO

Afisa Habari wa Simba, Haji Manara.

Afisa Habari wa Simba, Haji Manara ametoa ahadi kubwa kwa mashabiki wa klabu hiyo watakaojitokeza katika Uwanja wa Taifa leo itakapopambana na JS Saoura ya Algeria katika mchezo wa Klabu Bingwa Barani Afrika.


Katika mchezo huo, manara amesema kuwa atajichanganya pamoja na mashabiki katika siti za mzunguko ili kuwahamasisha kuishangilia timu yao ili ipate ushindi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Manara amesema, "watu wangu wa nguvu leo nakaa na nyinyi mzunguko!. Tunachinja mwanzo mwisho!, tunahanikiza wote kwa 'Yes We Can'!. Mniwekee nafasi upande wa kaskazini".

Simba inaanza kampeni yake ya hatua ya makundi ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika katika kundi la D, lenye timu za JS Saoura ya Algeria, AS Vita Club ya Congo na Al Ahly ya Misri.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527