Picha : TGNP MTANDAO YAENDESHA WARSHA KWA WAHARIRI KUHUSU BAJETI YA MRENGO WA KIJINSIA

TGNP Mtandao imeendesha warsha kwa Wahariri na baadhi ya waandishi wa habari kutoka mikoa mbalimbali nchini kuhusu bajeti yenye mrengo wa kijinsia kwa ajili ya kuwaongezea uelewa na uwezo kuhariri na kuripoti masuala ya kijinsia.

Warsha hiyo ya siku moja imefanyika leo Jumamosi Januari 19,2019 katika ofisi za TGNP Mtandao jijini Dar es salaam.

Akifungua warsha,Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao Lilian Liundi alisema mafunzo hayo yawawezesha wahariri na waandishi wa habari kuhamasisha uingizwaji wa masuala ya kijinsia katika mipango,miongozo na sera za serikali.

"Tumekutana hapa kwa ajili ya kukumbushana dhana kuu za jinsia na umuhimu wa kuzingatia masuala ya jinsia kwa maendeleo lakini pia kuweka mikakati ya namna ya kuongeza kasi ya kuripoti masuala ya kijinsia katika vyombo vya habari kwani tunaamini vyombo vya habari ni muhimu kwa maendeleo ya jamii",alisema Liundi.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao Lilian Liundi akizungumza wakati akifungua warsha ya wahariri kuhusu bajeti yenye mrengo wa kijinsia katika ukumbi wa ofisi za TGNP Mtandao jijini Dar es salaam. Picha zote na Kadama Malunde - na Frankius Cleophace Malunde1 blog
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao Lilian Liundi akizungumza wakati wa warsha hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao Lilian Liundi akielezea kuhusu dhana nzima ua bajeti yenye mrengo wa kijinsia.
Washiriki wa warsha hiyo wakiwa ukumbini.
Afisa Habari wa TGNP Mtandao Monica John akizungumza wakati wa warsha hiyo.
Washiriki wa warsha hiyo wakiwa ukumbini.
Afisa Habari wa TGNP Mtandao Monica John akisoma mwongozo kwa washiriki wa warsha hiyo.
Washiriki wa warsha wakiwa ukumbini.
Regina Mziwanda wa BBC Swahili akichangia hoja wakati wa warsha hiyo.
Warsha inaendelea..
Mhariri wa gazeti la Majira,Imma Mbuguni akichangia hoja ukumbini.
Afisa Habari Msaidizi wa TGNP, Jackson Malangalila akitoa mada kuhusu mawasilisho ya uchambuzi wa kijinsia wa bajeti kwa mwaka 2018/2019.

Afisa Habari Msaidizi wa TGNP, Jackson Malangalila akiendelea kutoa mada ukumbini.

Washiriki wa warsha hiyo wakiwa ukumbini.
Joyce Shebe kutoka Clouds Media akizungumza wakati wa warsha hiyo.
Mwandishi wa Habari Frankius Cleophace kutoka mkoa wa Mara akichukua matukio muhimu wakati wa warsha hiyo.
Jane Mihanji kutoka gazeti la Uhuru akiwa ukumbini
Warsha inaendelea.
 Picha zote na Kadama Malunde - na Frankius Cleophace Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post