DAWASA YAMTUA NDOO YA MAJI MAMA MARIA NYERERE


Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere akitoa shukrani zake mbele ya wageni waliohudhuria hafla ya kukabidhi tenki la maji nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere lililokarabatiwa na DAWASA hivi karibuni.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano DAWASA Neli Msuya akitoa ufafanuzi wa mradi huo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Cyprian Luhemeja akitoa maelezo juu ya mradi huo mbele ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (wa pili toka kushoto) na Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere pamoja wageni waliohudhuria hafla ya kukabidhi tenki la maji nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere lililokarabatiwa na DAWASA hivi karibuni.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (Katikati), akizungumza mbele ya wanahabari juu ya mradi wa ukarabati wa tenki la maji alilokabidhiwa Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere (kushoto). Pembeni ni Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Cyprian Luhemeja (kwanza kulia).
Wafanyakazi wa DAWASA, Wanahabari na wageni waalikwa wakisikiliza kwa makini.

Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere (kulia) akiwakaribisha Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (katikati) na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Cyprian Luhemeja (kwanza kulia) pamoja na wageni wengine waliokuwa wameambatana nao kukabidhi mradi wa tenki la maji lililokarabatiwa na DAWASA. Picha na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Kaimu Mkurugenzi wa miradi DAWASA Lydia Ndibalema akitoa maelezo machache kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (wa pili toka kushoto), Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Cyprian Luhemeja (kwanza kushoto) na Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere pamoja wageni waliohudhuria hafla ya kukabidhi tenki la maji nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere lililokarabatiwa na DAWASA hivi karibuni.
Kaimu Mkurugenzi wa miradi DAWASA Lydia Ndibalema akitoa maelezo machache kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (wa pili toka kushoto), Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Cyprian Luhemeja (kwanza kushoto) na Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere pamoja wageni waliohudhuria hafla ya kukabidhi tenki la maji nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere lililokarabatiwa na DAWASA hivi karibuni.
Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Cyprian Luhemeja akitoa maelezo machache kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange na wageni waalikwa


Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASA) mapema leo amekabidhi tenki la maji lenye ujazo wa lita 170,000 kwa mke wa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mama Maria Nyerere.

Tenki ambalo lilikuwa halitumiki na sasa litatumika na litawawezesha kupata maji nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere, Msasani jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Wanahabari mara baada ya kumaliza kukabidhi tenki hilo Msasani, jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Bodi ya DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange amesema wameamua kukarabati tenki hilo lilokuwa halitumiki kwa muda mrefu kutokana na miundombinu ya tenki kuwa chakavu nakupelekea kuwa na ukosefu wa maji ya kutosha nyumbani kwa Mama Nyerere.

Amesema maji ni kila kitu katika maisha ya binadamu hivyo hatuna budi kuyalinda na kuyatunza ili yaweze kututunza pia.

Nae Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere ameishukuru DAWASA kuweza kulikarabati tenki hilo lililokuwa limekufa na halitumiki kwa muda mrefu.

"Kiukweli sina cha kusema zaidi ya kutoa shukrani zangu za pekee kwenu kwa niaba ya mama yangu, hili tenki lilikuwa halitumiki kwa muda mrefu ila nyie mmelifufua na sasa tunapata maji ya kutosha," amesema Makongoro Nyerere.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema wao walijitoa kukarabati tenki hilo kwa kuondoa laini ndogo ya inchi moja ilikuwa inasababisha kutumia mota kuvuta maji ilikuwezesha kupata maji yakutosha hivyo kupelekea bili ya maji kuwa kubwa pamoja gharama za umeme.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527