MAHAKAMA YA KATIBA IMEANZA KUSIKILIZA RUFAA YA KUPINGA MATOKEO DRC

Mahakama ya Katiba katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo leo inaanza kusikiliza rufaa ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais wa Desemba 30.



Mahakama ya Katiba katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo leo inaanza kusikiliza ombi la kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais yaliyompa ushindi kiongozi wa upinzani, Felix Tshisekedi.

Ombi hilo limewasilishwa na mgombea mwengine wa upinzani, Martin Fayulu, aliyetangazwa kushika nafasi ya pili kwenye uchaguzi wa Desemba 30 ulioitishwa kumrithi Joseph Kabila.

Fayulu ameyaita matokeo hayo yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi, CENI, kuwa ni mapinduzi ya uchaguzi. Tshisekedi alitangazwa kupata asimilia 38.57 ya kura dhidi ya asilimia 34.8 za Fayulu.

Kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzio, CENI, mgombea aliyekuwa akiungwa mkono na Kabila alishika nafasi ya tatu akiwa na asilimia 23.8.

Hata hivyo, akitegemea matokeo yanayosemekana kukusanywa na mawakala wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki, CENCO, Fayulu anasema ni yeye aliyechaguliwa kwa zaidi ya asilimia 60 ya kura. Mahakama ya Katiba ina wiki moja ya kuamua juu ya madai ya Fayulu.

Chanzo:Dw

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527