MAKONDA "MNIOMBEE,NIKIKUA NIWE KAMA RAIS MAGUFULI"


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amewaomba viongozi wa dini wamuombee ili atimize ndoto ya kuwa kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli.

Muda mfupi uliopita akizungumza katika mapokezi ya ndege aina ya Airbus A220-300 uwanja wa ndege, Makonda amewataka viongozi wa Dini kumuombea juu ya ndoto yake ya kuwa kama Rais Magufuli kwa kuwa ni mtu wa kutekeleza.

"Viongozi wa dini naomba mniombee, nataka nikikua niwe kama Rais Magufuli, haya ni maombi yangu kabisa, kwa sababu ni mtu wa kutekeleza, usiyeyumbishwa,umehakiksha Mungu kwanza na unaipenda Tanzania kuliko hata familia yako"- Paul Makonda.

Makonda ameongeza, "hivi ulivyo Rais wetu angekuwa mwingine Watoto wake tungekuwa tunagombana nao mtaani lakini Wewe umehakikisha hakuna anayeingilia jukumu lako kama Baba wa familia" Makonda

Pamoja na hayo Makonda amemwambia Rais Magufuli, yeye na wakazi wa Dar es salaam wamekwenda kumuunga mkono kwa kuwa alitoa ahadi kutoka kwenye ilani ya CCM na anatekeleza ikiwemo elimu bure

"Nilipotoa tangazo la kuja hapa nilisema waje wale waliowahi kutoa ahadi na wakatekeleza" Makonda.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527