RAIS KENYATTA : MAGAIDI WALIOUA RAIA 14 NA KUJERUHI 30, WOTE WAMEUAWA


Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema magaidi wote waliofanya shambulio katika hoteli ya kifahari ya DusitD2 na kusababisha vifo vya watu 14, wameuawa.

Kenyatta ametoa kauli hiyo leo Jumatano Januari 16, 2019 wakati akihutubia Taifa kuhusu operesheni ya kupambana na magaidi waliovamia hoteli hiyo. Tukio hilo lililotokea jana Januari 15, 2019.

Amebainisha kuwa watu 700 wameokolewa na vyombo vya ulinzi na usalama, kwamba operesheni hiyo imekamilika na magaidi wote wameuawa.

Rais Kenyatta amesema watu 30 waliojeruhiwa walipelekwa katika hospitali mbalimbali za mjini Nairobi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post