MAMIA YA WATU WAANDAMANA MASHARIKI MWA MJI WA SUDAN

Mashuhuda wanasema kuwa majeshi ya ulinzi yametumia mabomu ya kutoa machozi kutawanya kundi la watu, ambao walikuwa wakiimbia wakisema Uhuru, Amani na Mapinduzi kwa Sauti ya Wananchi.


Maandamano hayo yaliandaliwa na Jumuiya ya Maprpfesa nchini Sudan, ambayo inamtaka Rais Bashir kujiuzulu.

Akizungumza katika kituo cha jeshi katika mji wa Atbara, kiongozi huyo amelaani kile alichokiita usaliti wa kuchoma mali kwa makusudi na kusababisha madhara.

Wakati huo huo Uingereza, Marekani, Canada na Norway zimetoa taarifa ya pamoja, zikisema kwamba zimeshtushwa na taarifa za vifo na kujeruhiwa kwa watu walioshiriki maandamano hayo ya kudai haki zao.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527