LORI LAGONGA TRENI DODOMA

Na.Alex Sonna,Dodoma
Watu wawili wamenusurika kifo baada ya lori aina ya scania walilokuwa wakisafiria kutoka Dodoma kwenda Iringa kuigonga treni ya mizigo katika makutano ya reli na barabara eneo la hazina jijini Dodoma.


Tukio hilo lilitokea jana mchana mara baada ya lori hilo lenye namba za usajili T463 ADW likiwa na tela lenye usajili T483 BLP kuiigonga treni hiyo iliyokuwa ikitoka jijini Dar es salaam kuelekea mikoa ya kanda ya ziwa.


Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo wamesema kuwa ajali hiyo imechangiwa na mvua zilizokuwa zikinyesha na kumfanya dereva wa lori kutoona kizuizi cha treni mbele yake.


Mmoja wa mashuhuda hao Ramadhani Rashid Mkazi wa Majengo amesema kuwa ajali hiyo ilichangiwa na dereva wa lori kutaka kukatiza kwa mwendo mkali lakini alikuwa kacheleWa hali iliyosababisha kugongwa na treni hiyo ya
mizigo.


“Dereva wa lori alikuwa katika mwendo mkali wakati akikatiza kivuko cha reli hivyo alishindwa kusimama na treni likawa limekaribia na kumgonga tumetoa watu wawili wakiwa wamejeruhiwa vibaya mwingine mmoja utumbo ukiwa nje”alisema


Kaimu kamanda wa polisi mkoani Dodoma ACP William Mkonda, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema chanzo ni uzembe wa dereva wa lori ambaye kwa sasa anashikiliwa na polisi na majeruhi wamelazwa katika hosipitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527