KIVUKO CHA MV MAGOGONI CHAPATA HITILAFU MAJINI,TEMESA YAOMBA RADHI

Leo tarehe 09/01/2019 mnamo saa 1:30 asubuhi kivuko cha MV. MAGOGONI kinachotoa huduma kati ya Magogoni na Kigamboni jijini Dar es Salaam kilipigwa na upepo mkali wakati kikikaribia upande wa Kigamboni. 

Hivyo, katika hali ya kupambana na upepo mitambo ya kuendeshea kivuko hicho iliingiliwa na takataka ambazo zilisababisha injini kupata moto na kupata hitilafu. 

Mafundi wetu wamefanikiwa kutatua hitilafu hiyo na huduma za kivuko hicho zimerejea katika hali ya kawaida mnamo saa 6:30 mchana. 

Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) unawaomba radhi abiria wote kwa usumbufu walioupata.

Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano
TEMESA
09/01/2019

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527