KIVUKO CHA MV MAGOGONI CHAPATA HITILAFU MAJINI,TEMESA YAOMBA RADHI
Wednesday, January 09, 2019
Leo tarehe 09/01/2019 mnamo saa 1:30 asubuhi kivuko cha MV. MAGOGONI kinachotoa huduma kati ya Magogoni na Kigamboni jijini Dar es Salaam kilipigwa na upepo mkali wakati kikikaribia upande wa Kigamboni.
Hivyo, katika hali ya kupambana na upepo mitambo ya kuendeshea kivuko hicho iliingiliwa na takataka ambazo zilisababisha injini kupata moto na kupata hitilafu.
Mafundi wetu wamefanikiwa kutatua hitilafu hiyo na huduma za kivuko hicho zimerejea katika hali ya kawaida mnamo saa 6:30 mchana.
Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) unawaomba radhi abiria wote kwa usumbufu walioupata.
Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano
TEMESA
09/01/2019
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin