KIUNGO WA CHELSEA AJIUNGA MONACO


Kiungo wa klabu ya Chelsea, Cesc Fabregas, amejiunga na klabu ya Monaco, kwa mkataba wa miaka mitatu na nusu.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 31 amejiunga na timu hiyo kuungana na nyota mwenzake wa zamani wa klabu ya Arsenal, Thienry Henry, ambaye kwa sasa ndio kocha wa Monaco.

Kiungo huyo tangu awasili Maurizio Sarri, katika klabu ya Chelsea, amekuwa na mgumu sana kupata nafasi tayari msimu huu ameanza michezo sita tu kwenye ligi kuu England.

Fabregas, ameshinda mataji mawili ya ligi kuu England ,na kombe la FA Cup mara mbili.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527