SINGIDA UNITED YASAJILI MAKOCHA WAWILI KUTOKA SERBIA

Uongozi wa klabu ya Singida United umeamua kuvunja benki kwa kuwasajili Makocha wawili kutoka Serbia kwa ajili ya kuifundisha timu hiyo.

Popadic Dragan ambaye ni Kocha Mkuu ameamua kuja na mwenzake ambaye atakuwa Msaidizi, Dusan Momcilovic.

Usajili wa makocha hawa umefanikiwa ikiwa ni baada ya klabu hiyo kutokuwa na Kocha Mkuu tangu kuondoka kwa Hans Van Der Plujim ambaye alitimkia Yanga.

Pengine Singida wameamua kuboresha benchi la ufnudi kwa ajili ya michuano ya SportsPesa Super CUP itakayokuja hivi karibuni.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527