BITEKO AFUNGUA MAFUNZO KWA WACHIMBAJI MADINI MKOANI MARA


Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (pichani) amefungua mafunzo ya siku mbili kuanzia leo Januari 04, 2018 kwa wachimbaji wadogo wa madini/ dhahabu yaliyofanyika katika Kijiji cha Byatika Kata ya Buhemba Wilaya ya Butiama mkoani Mara.

Mafunzo kama hayo yanaendelea kwa nyakati tofauti katika maeneo mbalimbali nchini ambapo juzi Januari 02, 2018 Biteko alifungua mafunzo kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu/ madini katika Wilaya ya Bukombe mkoani Geita.

Mafunzo hayo yanatolewa na Serikali kupitia taasisi zake ikiwemo Tume ya Madini pamoja na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ombi la wachimbaji wadogo wa madini hapa nchini ambao waliomba kupatiwa mafunzo ili kufanya shughuli zao kwa weledi bila kubahatisha.

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Afisa Madini mkoani Mara, Nyaisara Mgaya akifafanua jambo wakati wa mafunzo hayo.
Godson Kamihanda kutoka Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini hapa nchini (GST) akizungumza wakati wa mafunzo hayo ambapo katika mafunzo hayo taasisi hiyo itatoa taarifa ya utafiti wa madini hapa nchi ili uwasaidie wachimbaji kufanya kazi zao bila kubahatisha.
Wachimbaji wadogo wa dhahabu wakifuatilia kwa umakini mafunzo hayo.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (aliyekaa kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika wilaya ya Butiama mkoani Mara.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (aliyekaa kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika wilaya ya Butiama mkoani Mara.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (aliyekaa kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika wilaya ya Butiama mkoani Mara.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (aliyekaa kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika wilaya ya Butiama mkoani Mara.
Awali Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko alipita katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya Butiama, Anna Rose Nyambi (pichani) na kupokea taarifa ya hali ya uchimbaji madini katika wilaya hiyo.
Tazama BMG Online TV hapa chini


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527