AMRI SAIDI APEWA HESHIMA YA UKOCHA BORA


Dismas Ten na Amri Said
'Huwezi kukataa, Amri Said ni kocha mzuri na bora lakini pia ameongeza kitu ndani ya Biashara United'', maneno ya Dismas Ten msemaji wa Yanga baada ya timu yake kupangwa na Biashara kwenye mchezo wa raundi ya 4 ya kombe la shirikisho.

Dismas amempa heshima hiyo Amri Said ambaye katika mchezo wake wa kwanza tu tangu awe kocha wa Biashara United alishinda 2-1 dhidi ya Mbeya City, hivyo Ten amekiri kuwa Amri Said ameibadilisha timu hiyo.

''Tumepangwa kucheza nyumbani dhidi ya Biashara United, mchezo utakuwa mgumu ukizingatia mabadiliko ya benchi la ufundi ambayo wamefanya Biashara lakini pia lazima uzingatie kuwa waliifunga timu gani'', ameongeza Dismas.

Yanga ambao ni mabingwa wa michuano hiyo msimu wa 2015/16 wametinga raundi ya 4 baada ya kuwatoa Tukuyu Stars ya Mbeya kwa mabao 4-0 huku Amisi Tambwe akifunga Hat-trick.

Amri Said aliifundisha Lipuli FC msimu wa 2017/18 na kuisaidia kumaliza katika nafasi ya 7 ikiwa na alama 38. Msimu huu aliuanza na Mbao FC kabla ya kuachana nayo mwezi Desemba na kujiunga na Biashara United.
Via >>EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527