DIWANI AJIUA KWA KUTUMIA MTANDIO


Diwani wa zamani wa kata ya Nyerere, Unguja Asha Ali Abei amejinyonga hadi kufa usiku wa kuamkia leo Jumatano Desemba 26, 2018.

Akizungumza leo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja, Kheri Musa amesema marehemu ambaye kwa miaka ya nyuma alikuwa diwani, alikutwa amekufa kwa kujinyonga akitumia mtandio alioufunga katika dirisha, tukio lililotokea katika shehia ya Magomeni.

Baadhi ya majirani wa marehemu walisema kwamba walipata taarifa za kifo hicho asubuhi baada ya mtoto wa marehemu kupiga kelele.

Sheha wa shehia ya Magomeni, Rajab Ali Ngauchwa amesema si vyema wananchi kuchukua hatua za haraka katika mambo yanayowachanganya.

Amesena ni vyema familia kukutana na kujadili ili kupata ufumbuzi wa tatizo kuliko watu kuchukua uamuzi kama huo wa kujitoa uhai.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527