DE GEA KUONGEZA MWAKA MMOJA NA MASHETANI WEKUNDU

Manchester United wametumia kifungu kwenye mkataba wa kipa wao David de Gea kinachowaruhusu kumuongezea mkataba kumuongezea mkataba wa mwaka mmoja.


Wamechukua hatua hiyo kuondoa utata kuhusu mustakabali wake, dirisha ndogo la kuhama wachezaji litakapofunguliwa Januari.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania alijiunga na United kutoka Atletico Madrid mwaka 2011.

Mkataba wa sasa wa De Gea, 28, unafika kikomo mwisho wa msimu, jambo ambalo lingempa fursa ya kuanza kuzungumza na klabu nyingine kuanzia Januari 1 au hata kuingia kwenye mkataba wa awali.

Hata hivyo, United sasa wameamua kurefusha mkataba wake kwa mwaka mmoja.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527