MANARA AWATISHIA NYAU NKANA RED DEVILS....ASEMA UJINGA NI WAKATI WA KWENDA TU


Afisa Habari wa Mabingwa watetezi nchini, Haji Manara, ameweka wazi kwamba ni lazima ushindi upatikane siku ya leo kwa klabu ya Simba dhidi ya Nkana FC ya Zambia kwenye mashindano ya Klabu bingwa Afrika.

Manara amesema hayo ikiwa yamebaki masaa machache ili timu hizo kuweza kukutana katika uwanja wa Taifa ikiwa ni mchezo wa marudiano.

"Ujinga wakati wa kwenda tu,wakati wa kurudi hata wajishike Ugoko lililoandikwa litakuwa tu Insha'Allah. Kufa au kupona", Manara.

Ujumbe huo wa Manara umekuja kufuatia wachezaji wa Nkana Red Devils kuingia uwanjani wakiwa wamejishika kichwani kila mmoja ishara ya kujikuna hivyo Manara amesema kwa hapa hata wakishika ugoko watawafunga tu.

Mchezo wa kwanza wa Simba na Nkana uliochezwa Kitwe, Zambia ulimalizika kwa wekundu wa msimbazi kukubali kupokea kipigo cha mabao 2-1.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527