KARIA:TUPO MBIONI KUMPATA MDHAMINI MKUU WA LIGI 2018/2019

Rais wa shirikisho la soka nchini Tanzania(TFF) Wallace Karia amesema wamekuwa kimya kwa muda mrefu kwa kuhofia kuharibu mipango ambayo wanaendelea nayo lakini sasa wamefikia pazuri na muda wowote wanaweza kupata mdhamini mkuu wa ligi.

''Kuhusu mdhamini tumefikia pazuri, hivi karibuni tulikuwa mjini Durban Afrika Kusini, tumeongea na kampuni moja ambayo inafanya shughuli zake hapa nchini kwahiyo tupo kwenye hatu nzuri ya kupata mdhamini'', amesema Karia.

Karia amesema sababu za kujitoa mdhamini aliyekuwepo kampuni ya Vodacom ni kwasababu walishusha kiwango cha fedha na wao kama TFF hawakuwa tayari kuendelea nao kulingana na thamani ya ligi hivyo wakaachana.

Ligi kuu soka Tanzania bara ambayo ipo katika raundi ya 13 inaendelea bila kuwepo kwa mdhamini mkuu hivyo hata zawadi ya bingwa bado haijawekwa wazi.

Chanzo:Eatv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527