MO DEWJI AITAKIA KILA LA KHERI TAIFA STARS DHIDI YA LESOTHO

Mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania, Mo Dewji ametoa salamu za kheri kwa Timu yetu ya Taifa ya mpira wa miguu, Taifa Stars katika kuelekea mchezo wa kufuzu AFCON dhidi ya Lesotho.

Dewji amesema kuwa ushindi wa leo dhidi ya Lesotho utaleta furaha kubwa kwa Watanzania, kwani ni miaka 38 tangu timu ya taifa ifuzu michuano hiyo kwa mara ya kwanza.

“Nawatakiwa kila la kheri Taifa Stars katika mchezo wa leo dhidi ya Lesotho. Ushindi wa leo utarudisha furaha ya Watanzania ya kukosa kushiriki AFCON kwa miaka 38. Tunaamini mtafanya vizuri sababu nia tunayo na uwezo tunao. Mungu awe nanyi,“ameeleza Mo Dewji kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527