LUSINDE ATAKA KOCHA WA TAIFA STARS, EMMANUEL AMUNIKE AFUKUZWE KAZI

Mbunge wa Mtera kupitia CCM, Livingstone Lusinde amelitaka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuandaa barua ya kumfukuza kazi kocha wa Taifa Stars, Emmanuel Amunike ili akishuka nchini akabidhiwe akitua tu uwanja wa ndege.


Lusinde (Kibajaji) ametoa kauli hiyo kufuatia matokeo ya jana ambapo Taifa Star ililala kwa bao 1-0 kutoka kwa Lesotho na kujiweka katika mazingira magumu ya kufuzu kwa Afcon 2019, Cameroon.


"Hii serikali mawaziri wanatumbuliwa wakikosea kidogo tu, sasa huyu kocha anazoa wachezaji na kuwapanga anavyotaka yeye halafu tumwache, namuomba Waziri Mwakyembe awaandikie TFF akiwa huko ili wavunje haraka mkataba," alisema Lusinde


Mbunge huyo alisema Kocha wa Taifa Stars, Amunike amekuwa na upendeleo wa upangaji wa kikosi na badala yake anapanga watu kwa kuangalia matakwa ya wapenzi siyo kitaalum.


Kibajaji alisema sifa ya kocha wa Tanzania ni nidhamu kwa wachezaji ambayo watafundishwa jeshini, lakini suala la soka limemshinda.


Licha ya kuelezwa bado kuna tumaini la kusonga mbele, lakini Kibajaji alisema ndoto imeanza kufifia kwani timu ya Uganda iko vizuri wakati washindani wetu wanakutana na timu ambayo haiwezi kushindana.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527