MAJAY AMTOLEA MAHARI LULU MICHAEL

Malkia wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ siku ya jana anadaiwa ametolewa mahari na mpenzi wake wa muda mrefu Majay ikiwa ni maandalizi ya ndoa yao mwisho wa mwaka huu.


Mrembo huyo amefanya sherehe hiyo ikiwa ni siku chache toka amalize hadhabu yake ya kifungo cha miaka 2 jela baada ya kukutwa na hatia na mahakama ya kumuua Steven Kanumba bila kukusudia.


Katika video ambazo zinasambaa mtandaoni zinamuonyesha mrembo huyo akimtambulisha mume wake huyo mjarajiwa kwa wazazi wake.

Mkuu wa Mkoa Wa Dar Es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda katika ukurasa wake wa instagram atoa pongezi kwa kuandika, “Mafanikio yenu yamebeba watu wengi, na kila hatua inaonyesha hamtanii basi Mungu wangu aendelee kuwaonyesha njia ili mfikapo mkawe msaada na kwawengine.”

Mastaa kibao walikuwepo kuhudhuria sherehe hiyo ya kutolewa mahali kwa Lulu jambo ambalo ni hatua mpya kuelekea ndoa yao inayotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527