MTOTO ALIYETEKWA KIMAFIA DAR AFIKISHA SIKU 60, AKOSA MITIHANI


Dar es Salaam. Idrissa Ally (13), mwanafunzi wa darasa la tano Shule ya Msingi Princes Gate jijini Dar es Salaam hadi jana mchana alikuwa ametimiza siku 60 tangu alipotekwa kwa staili ya ‘kimafia’ akiwa anacheza na wenzake na kumfanya akose mitihani ya mwisho wa mwaka.

Wakati mwalimu mkuu wa shule hiyo, Mussa Idrissa akisema mitihani ilianza Novemba 19 kwa wanafunzi wa darasa la kwanza, pili, tatu, tano na sita, Ally Idd, baba mzazi wa Idrissa amesema wanaendelea na maombi ili mwanaye arudi salama.

Idrissa alitekwa Septemba 26 saa 11 jioni akiwa anacheza na wenzake eneo la Tegeta Masaiti wilayani Kinondoni.

Alichukuliwa na dereva mwanaume aliyekuwa katika gari aina ya Toyota IST, ambaye alitoa kichupa kidogo kinachodhaniwa ni ‘spray’ na kumpulizia mtoto huyo na kumuingiza mlango wa nyuma wa gari na kuondoka naye.

“Bado Idrissa anakumbukwa na wanafunzi wenzake, nakumbuka wakati tunawatangazia kuanza kwa mitihani hii, mmoja wa wanafunzi anayeitwa Amran alimuuliza mwalimu wake wa darasa kama Idrissa atakuja kufanya mtihani,” alisema Mussa.

“Mwalimu akamjibu kuwa Idrissa atafanya mitihani kama kawaida.”


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527