BARAZA LA MITIHANI - NECTA LIMEFUTA MATOKEO YA MTIHANI DARASA LA SABA 2018 KWA SHULE HIZI


Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) limefuta matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya shule ya msingi baada ya kubainika kuvujisha mtihani huo uliofanyika Septemba 5 na 6, 2018.

Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Oktoba 2, 2018 amezitaja shule zilizofutiwa matokeo ni za halmashauri ya Chemba, Kondoa mkoani Dodoma.

Zingine ni Hazina na New Hazina, Aniny Nndumi na Fountain of Joy za jijini Dar es Salaam na Alliance na New Alliance na Kisiwani zote za Mwanza.

Dk Msonde amesema baada ya uchunguzi shule hizo zimebainika kuvujisha mitihani hiyo iliyofanyika Septemba 5 na 6 wakishirikiana na waratibu wa elimu wa eneo husika.

Akizungumzia wilaya ya Chemba, Dk Msonde amesema uongozi wa idara ya elimu ya halmashauri hiyo ulipanga kufanya udanganyifu kupitia waratibu wa elimu na wasimamizi kuhakikisha ufaulu unaongezeka.


"Uongozi uliandaa makundi ya ‘WhatsApp’ yaliyojulikana kama jina elimu Chemba, sayansi na hesabu na wasimamizi wa elimu Chemba. Makundi haya yaliwajumuisha waratibu wa elimu kata na baadhi ya wakuu ili kurahisisha mawasiliano baina yao,” amesema

Na Bakari Kiango,Mwananchi 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527