DC CHUNYA AKUTANA NA WACHIMBAJI WADOGO NA KUSIKILIZA KERO ZAO


Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhandisi Meryprisca Mahundi (kushoto) akisikiliza meelezo kutoka kwa mmoja wa wachimbaji wadogo wa madini eneo la mara baada ya kufanya ziara katika eneo hilo ili kusikiliza kero na changamoto zinawakumba wachimbaji hao. 
Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhandisi Meryprisca Mahundi (katikati)akisikiliza maelezo kutoka kwa kwa mmoja wa wachimbaji wadogo katika eneo la usafishaji madini aina ya dhahabu.
Ziara ya ukaguzi wa maeneo ya uchimbaji wa madini katika eneo la wachimbaji wadogo wa dhahabu ambapo mkuu wa Wilaya hiyo Mhandisi Maryprisica Mahundi alipata fursa ya kuzungumza na baadhi ya wachimbaji wadogo na kutambua changamoto wanazo kutana nazo. 
Baadhi ya akina mama wanaojihusisha na shughuli za uchimbaji madini wakifurahi jambo mara baada ya kutembelewa na Mkuu wa Wilaya ya Chunya Meryprisca Mahundi ambaye amefanya ziara katika maneo ambako kunafanyika shughuli za uchimbaji madini ,ziara hiyo inalengo la kusikiliza na kutambua kero zinazowakabili wachimbaji hao. 
Ahobokile Mwasyeba (katikati)mmoja wa wachimbaji wadogo katika eneo la Chokaa Wilayani Chunya Mkoani Mbeya akitoa maelezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhandisi Meryprisca Mahundi namna ambayo shughuli ya uchimbaji dhahabu unavyofanyika. 
Shughuli za uchimbaji madini zikiendelea kwa wachimbaji wadogo eneo la Chokaa Wilayani Chunya Mkoani Mbeya. 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527