IDADI YA WALIOFARIKI KWENYE KIVUKO YAFIKIA 196



Saa 7:28 Septemba 22,2018

Idadi ya watu walioopolewa ziwani yafikia 196 zoezi la uopoaji na uokoaji linaendelea.


Saa 5:22 Asubuhi Septemba 22

Mhandisi wa Kivuko cha Mv.Nyerere kilichopata ajali ya kuzama ziwa Victoria .Alphonce Charahani ameokolewa muda mfupi uliopita akiwa hai japo hali yake ni mbaya lakini anapatiwa huduma.

Imeelezwa fundi huyo alikuwa amekwama kwenye moja ya vyumba vya manahodha na alikuwa akigongagonga vitu ili waokoaji wamsikie jambo ambalo limetimia.

Lakini hawezi kuongea kutokana na hali yake kuwa mbaya baada ya kukaa ndani ya maji kwa takribani siku tatu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527