MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MSALALA SIMON BEREGE APATA AJALI YA GARI MLIMA SEKENKE

Mkurugenzi wa halmashauri ya Msalala, Simon Belege na mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Mibako Mabubu wamenusurika kifo baada ya gari walilokuwa wamepanda kugonga ng’ombe katika mteremko wa Mlima Sekenke.

Viongozi hao walikuwa wakitokea mkoani Dodoma kuelekea Igunga, Tabora kuwahi kikao cha utekelezaji wa ilani ya CCM kitakachofanyika kesho Jumamosi Septemba 15, 2018.

Katika gari hilo, Mkurugenzi huyo alikuwa pamoja na mwenyekiti wa halmashauri hiyo, mweka hazina, Masatu Mnyoro na mwanasheria wake, Mashaka Mabula.


Majeruhi wa ajli hiyo wamelazwa katika Hospitali ya Igunga mkoani Tabora wakiendelea kupatiwa matibabu.

Mganga mkuu wa hospitali hiyo, Bonaventura Kalumbete amesema Belege na Mabula ndiyo waliokuwa wamelazwa lakini baada ya kuwapatia matibabu hali zao zinaendelea vizuri na wakati wowote wataruhusiwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527