BABA LEVO APANDISHWA KIZIMBANI


Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva Craython Revocatus Chipando, maarufu kama Baba Levo aliwasili mapema leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Kigoma kusikiliza hukumu ya kesi inayomkabili.

Msanii huyo ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mwanga Kaskazini kwa tiketi ya ACT Wazalendo anatuhumiwa kufanya makosa matatu ikiwemo kutumia lugha ya matusi, kumshambulia na kumfanyia vurugu muuguzi wa zahanati ya Msufini iliyopo kata ya Mwanga Kaskazini.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi terehe 19, Septemba mwaka huu.

Chanzo : Azam TV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post