MAGUFULI: VIONGOZI DAR MJITAFAKARI....HAKUNA MWENYE GARANTII YA KAZI


Rais John Magufuli, amewataka viongozi wa Jiji la Dar es salaam, wametakiwa kujitafakari katika utendaji kazi wao kwani imeonekana kukwama katika sekta mbalimbali ikilinganishwa na majiji mengine.

Kauli hiyo ameitoa leo katika hafla ya uapishwaji wa viongozi walioteuliwa wakiwamo Wakatibu wa Wakuu wa wizara mbalimbali, Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala iliyofanyika Ikulu jijini.

Rais Magufuli amesema kumekuwa na ‘upigaji’ mkubwa huku viongozi wakiangalia bila kuchukua hatua zozote.

“Juzi nilikuwa naongea na mabalozi, nikawaambia Dodoma ndiyo inaongoza katika majiji, manispaa, wilaya Tanzania nzima hivyo unaweza ukajiuliza kuna nini unaweza ukajua hapa Dar es salaam kuna upigaji na viongozi wapo,” amesema Magufuli.

Amesema viongozi wa Dar es salaam wakikutana kwenye vikao wanakaa siku mbili lakini zitajazwa ni siku nne hivyo kwa namna hiyo hawawezi kupata mapato kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

“Utakuta hata wamachinga wanasimama barabarani hawana mahali pa kufanyia biashara, wakina mama wamedhulumiwa lakini viongozi wapo hivyo nataka niwaambie viongozi mlioteuliwa hakuna mwenye garantii ya kazi,” amesema Rais Magufuli.

|Anna Potinus - Mtanzania Dar es Salaam

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527